.

Jumanne, 1 Novemba 2016

Hamisa Mobetto afunguka kuhusu bifu lake na Zari

14719814_205719963185870_2786780441858801664_n

Hamisa Mobetto amefunguka juu ya mahusiano yake na first lady wa Madale, Zari The Bosslady baada ya tetesi za kutoka na Diamond.
Mrembo huyo amemuambia mtangazaji wa kipindi cha The Playlist cha Times FM, Omary Tambwe aka Lil Ommy kuwa hajawahi kuwa na urafiki na Zari na wala hawana uadui wowote.
“Unajua huwezi kusema kuwa mimi na Zari tuko sawa au hatupo sawa kwa sababu hatujawahi kuwa marafiki, na mimi nimemjua kwa sababu ‘Kazaa’ na bosi wangu [Diamond Platnumz],” amesema Hamisa.
Malkia huyo wa video ya Salome ameongeza kuwa amewahi kuonana na Zari mara moja pekee ambapo ilikuwa ni kwenye 40 ya Tiffah mwaka jana.

Bonyeza HAPA kudownload application yetu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni