.

Alhamisi, 3 Novemba 2016

Femi One ataja wasanii wa Tanzania anaotamani kufanya nao kazi

Rapper wa kike kutoka Kenya, Femi One amewataja wasanii wa Bongo Flava ambao anatamani kufanya nao kazi.
14736394_193523564429838_6064226361453576192_n
Akiongea na Bongo5, Femi amewataja wasanii hao kuwa ni pamoja na G-Nako, Joh Makini na Ruby.
“Napenda kufanya kazi na Joh Makini kutokana na anavyochana, Gnako anavyoflow kwa style nyingi. Msanii mwingine ni Ruby, naipenda sauti yake lakini pia nampenda Nay wa Mitego alivyokuwa haogopi kutaja watu kwenye nyimbo zake,” amesema Femi.
Mpaka sasa rapper huyo ameshaachia video mbili ikiwemo ‘Jah’ na yupo chini ya lebo ya Kaka Empire inayomilikiwa na King Kaka.

Bonyeza HAPA kudownload application yetu na upate habari punde zinapotufikia

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni