.

Jumanne, 8 Novemba 2016

Donald Trump na Hillary Clinton kujinadi kwa mara ya mwisho

Hillary Clinton na Donald Trump wamefanya mikutano ya dakika za mwisho mwisho kuwahimiza raia wa Marekani wawapigie kura zikiwa zimesalia saa chache kabla ya uchaguzi kufanyika.
Wote wawili wamefanya mikutano ya kampeni katika majimbo ya kushindaniwa ya Carolina Kaskazini, Pennsylvania na Michigan.
Bi Clinton amewahimiza wapiga kura kuunga mkono kuwepo kwa "Marekani yenye matumaini, inayojumuisha wote na yenye ukarimu".
Bw Trump naye amewaambia wafuasi wake kwamba wana "fursa nzuri ya kuvunja mfumo mbovu na usio na maadili".
Kura za maoni zinaonesha Bi Clinton wa chama cha Democratic akiwa asilimia nne mbele ya mpinzani wake Bw Trump wa chama cha Republican.

Bonyeza HAPA chini kudownload application yetu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni