.

Jumanne, 14 Juni 2016

Baby Madaha awaponda waigizaji wa kike waliopo katika mapenzi na wanaume wa umri mdogo


Mwigizaji wa filamu za Bongo, Baby Joseph Madaha ‘Baby Madaha’, ameibuka na kudai kwamba anashangazwa na waigizaji wa kike waliopo katika mapenzi na wanaume wa umri mdogo.

Baby Madaha ambaye ameolewa na Mwarabu wa Dubai, amesema tabia ya wasanii wenzake kuwa na wanaume wenye umri mdogo maarufu ‘Serengeti Boys’ unafedhehesha na haiwasaidii chochote zaidi ya kujishushia hadhi yao.

Baby Madaha aliongeza kufafanua kwamba, tabia iliyojengeka kama fasheni kwa wasanii wakike watu wazima kuwa na wanaume wenye umri mdogo bila aibu wala kujifikiria athari zake ikiwemo kujishushia hadhi zao.

“Sijawahi kuwaza kama nitakuwa na Serengeti boy kwangu hawana nafasi sioni faida yoyote kwao, mimi nawashangaa kwa kuwa wengi wao wanatafuta umaarufu hakuna mapenzi wala maisha endelevu hapo,” alifafanua Baby Madaha.

Hata hivyo, Baby Madaha, aliongeza ushauri wake kwa kuwataka wasanii wenzake kuwa na wanaume wenye umri wao ama wawe na wanaume watu wazima kama wanataka kulinda heshima zao na kujiongezea mashabiki badala ya kuwa na wanaume wenye umri mdogo.

Baadhi ya wanawake wasanii walio katika uhusiano wa kimapenzi na wanaume wenye umri mdogo ni pamoja na Wema Sepetu (28) na Idrissa (22), Zari (36) na Diamond (27), Aunty Ezekiel (30) na Iyobo, Jaquline Wolper (29) na Harmonize.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni