.

Ijumaa, 23 Desemba 2016

QUEEN DARLEEN ASEMA HANA BAHATI YA KUDUMU KWENYE MAPENZI


Mkali toka WCB the firstlady herself Queen Darleen anayetamba na ngoma kali kitaa ya Kijusokafunguka kupitia Amplifaya ya Clouds fm leo hii kwenye interview na Minah kwamba yeye hana bahati ya kukaa na mwanaume,akikaa na mwanaume kidogo tu badae wanatofautiana kiasi kwamba anaamini kwamba hasara yake kubwa ni mapenzi Queen Darleen anasema
Sina bahati ya kukaa na mwanaume, kila mwanaume nikikaa naye baadaye tunakuja kutofautiana, hicho ndio kitu kikubwa kwasababu pesa najua kutafuta, kama maisha ninayoishi ni ya kawaida kama watu wengine wanavyoishi”
Kutokana na muonekano alionao queen Darleen,Minah akauliza isije ikawa unachagua sana kwasababu mwonekano wako ni kama wale wa mateke na ngumi, queen Darleen alikua na jibu hili
Cha kwanza mimi siangalii mwanaume ananipa nini,siangalii mwanaume anasifa gani, sijali uwe na kazi au hauna, uwe na maisha mazuri au hauna, hata kama haunipendi nitakuforce tu mpaka unipende, na katika maisha yangu sipendi mwanaume anayenitongoza, napenda mwanaume nimfate mwenyewe” alimaliza hivyo mkali huyo kutokaWCB
Bonyeza HAPA kudownload application yetu

Bonyeza HAPA kusubscribe katika YouTube channel yetu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni