.

Ijumaa, 18 Novemba 2016

RwandAir kununua ndege mpya aina ya Boeing 737-800 Next Gen

14793389631

Huduma za usafiri wa ndege zinazidi kushika kasi kwenye mataifa ya Afrika Mashariki kila siku, Kutoka nchini Rwanda nimeipata hii ya Shirika la ndege la Rwanda, RwandAir kununua ndege mpya aina ya Boeing 737-800 Next Gen ambayo inatarajiwa kuongeza ushindani wa safari za anga duniani .
RwandAir imekuwa kampuni ya kwanza barani Afrika na ya pili duniani kununua ndege ya aina hiyo ambayo imewekwa vifaa vya kuwezesha abiria kutumia huduma za intaneti kwa njia ya Wi-Fi.
Ndege hiyo ina uwezo wa kubeba abiria 154 ilitolewa oda ya kununuliwa na Rwanda miaka 6 iliyopita, imetua kwenye uwanja wa ndege wa Kigali November 16, 2016 saa 10 usiku.
Waziri wa uchukuzi wa Rwanda Alexis Nzahabwanimana, amesema ndege hiyo mpya itawezesha shirika hilo kupanua safari zake barani Asia, Ulaya na Marekani.
Mwezi September mwaka huu, Serikali ya Rwanda ilinunua ndege nyingine ambayo ni ya kwanza Afrika Mashariki aina ya Airbus 330-200, iliyopewa jina la ‘Ubumwe’ ikiwa na maana ya Umoja.
14793389631
1475012201ra-toulouse-2
14793400521John Mirenge, Mkugenzi Mtendaji wa Rwandair’s CEO akiitambulisha ndege hiyo iliyopewa jina la ‘Kalisimbi’.
14793401531
14793402571
14793403221
14793404351
14793405861Dr Alexis Nzahabwanimana, Waziri wa Usafirishaji akizungumza wakati wa mapokezi ya ndege hiyo.

14793407271

14793399771
14793408721

Download application yetu HAPA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni