.

Jumapili, 9 Oktoba 2016

Young Dee afunguka kuhusu ujio wake mpya


Young Dee ameamua kufunguka kwa mashabiki wake kwamba mwaka huu ni wakati wake kuja kivingine.
Rapper Young Dee anayetamba na kibao chake cha“Hands Up” ameamua kufunguka kwamba anataka kumwondoa yule Young Dee wazamani katika vichwa vya watu na kuwaletea Young Dar es salaam mwingine kabisa ambaye hayupo vichwani mwa mashabiki zake.
Kupitia kipindi cha Ngaz kwa Ngaz, Young Deeamesema kwamba baada ya kutangaza rasmi kuachana na madawa ya kulevya, amesema kwamba hadi mfumo wake wote wa kuishi ameubadili na nitofauti kabisa na ule aliokuwa nao mwanzo
“Mfumo wangu wote wa maisha ulikuwa haupo sawa hivyo Chochote nachofanya saizi kama hakinipeleki kwenye siku yangu ya mafanikio basi hakina nafasi kwenye maisha yangu, ni vitu ambavyo naamua mimi mwenyewe kama mtoto wa kiume kuna muda naamua kuwa hiki ni kwa ajili ya maisha yangu, mimi hapa nina Mama yangu na familia inaniangalia hivyo maamuzi niliyoamua ni kuikana nafasi yangu, yaani nataka nimuuwe yule Young D wa zamani pia nimlete huyu Young D mpya ambaye huyu mpya atawafanya watu wamsahau yule wa zamani kama aliwahi kuwepo”alisema Young Dee

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni