.

Jumatano, 26 Oktoba 2016

Pesa utatakiwa kulipa Ili upate Collabo na Akothee

akoth
Kama ilivyo ahadi yangu kwako, ni kuhakikisha haipitwi na story yoyote mtu wangu na leo nimeipata hii kutoka kwa msanii wa muziki kutoka Kenya, Akothee. Inawezekana wengi wetu tunafahamu tu kwamba ni msanii na labda kwasababu ana historia ya kuwa na pesa nyingi basi hata muziki anaufanya tu kama starehe. 
Kwa mujibu wa Citizen, taarifa hii ikufikie kama ni msanii na unahitaji kufanya collabo na Akothee basi unatakiwa kuandaa mfuko wako kisawasawa. Akothee ametangaza kiwango cha Pesa ambacho utatakiwa kumlipa ili uweze kuingia naye studio kuwa ni Shilingi Milioni 1 za Kenya ambazo ni zaidi ya shilingi Milioni 21 za Tanzania.
“Ukiwa msanii, hautakiwi kukimbilia kusaini deal za record labels, uanweza kutengeneza pesa zako kuoitia social media. Usijikalishe na kusubiri pesa zije. Sasa kwa upande wangu wala usijisumbue kunipigia simu kama hauna shilingi Milioni 1 za kufanya collabo,” –Akothee
Akothee amesema anatafikiria kusaini deal na lebel za Marekani endapo tu zitakuwa na maslahi ya kueleweka. 
Star huyo wa single ya ‘Yuko Moyoni’ hivi karibuni amefanikiwa kushinda tuzo mbili za best East African female artist zilizotolewa na waandaaji wa jarida la African Muzik Magazine (AFRIMMA) pamoja na African Entertainment Awards USA (AEAUSA).
akothee1
Perhaps it is the awards that have inflated the cost of doing a collabo with her!
akoth

Download application yetu na upate habari punde zitufikiapo HAPA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni