.

Jumatatu, 16 Mei 2016

GIGY MONEY:NIPO KWENYE MAHUSIANO NA GARDNER MIEZI 6 SASA

MUUZA sura kwenye video za Kibongo, Gift Stanford ‘Giggy Money’ amefunguka kuwa mtangazaji maarufu Bongo wa Clouds FM, Gardner G. Habash hachomokikwake na hadi sasa wako kwenye uhusiano wa mapenzi kwa muda wa miezi sita.

Gigy mefunguka haya baada ya picha zinazomuonesha akiwa kwenye mapozi yakimahaba na Gardner kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.

Giggy alisema mtangazaji huyo amekuwa mtu wa muhimu kwake kwa sasa.“Kwani kuna tatizo nikiwa na Gardner?
Yule ni mtu muelewa na sahihi kwangu, ninafikiri kupitia yeye nitajifunza mambo mengi na kuzidi kufanikiwa kwa sababu yeye ni moja kati ya watu ambao wako kwenye tasnia ya burudani kwa muda mrefu,” alisema Giggy Money.Gardner alipotafutwa ili aweze kueleza kuhusu ishu hii alisema:“Nipo karibu na Giggy lakini hatuna uhusiano wa kimapenzi, kwa hiyo kama anasema hivyo si kweli lakini yeye ni shabiki wangu na mimi ni mshabiki wake, ninapenda pia kazi anazozifanya,”.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni