.

Jumatano, 26 Aprili 2017

Rais JPM Atoa Msamaha kwa Wafungwa 2,219


Rais John Magufuli leo ametoa msamaha kwa wafungwa 2,219 ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani, Projest Rwegasira inaeleza kuwa wafungwa hao ni wale wenye magonjwa kama Ukimwi, saratani na Kifua Kikuu na wazee wenye umri wa kuanzia miaka 70.

“Ni mategemeo ya Serikali kwamba watarejea tena katika jamii kushirikiana na wenzao katika ujenzi wa Taifa na kwamba watajiepusha kutenda makosa ili wasirejee tena gerezani.” Imesema taarifa hiyo

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia FacebookTwitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka HabNews Tv

Bonyeza HAPA kupakua application yetu na upate habari punde zitufikiapo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni