.

Jumanne, 18 Oktoba 2016

Martin anataka alipwa $130,000 kila mwezi na Mary J. Blige

3978d12200000578-3845996-image-a-31_1476754612469
Mume wa Mary J. Blige, anataka awe analipwa $130,000 (zaidi ya shilingi milioni 286) kila mwezi ili zimsaidie kuendelea kuishi maisha ya kifahari aliyokuwa akiyafurahia kabla ya MJB hajaomba talaka.
3978d10e00000578-3845996-image-a-27_1476754589744
Martin ‘Kendu’ Issacs, 49, anaamini kuwa mwanamuziki huyo wa R&B anapaswa kumsaidia kulipia gharama za mazoezi, mpishi binafsi na posho ya $1,000 kwaajili ya kununua nguo mpya.

Blige, 45, aliomba talaka kwa Issacs July, akisema ni kutokana na tofauti zisizosuluhishika baada ya kukaa kwenye ndoa kwa miama 13. Pia alimtimua kama meneja wake na kumwacha bila chanzo cha kuingiza pesa.
Katika malalamiko yake kortini, Isaacs anadai alikuwa akiingiza $46,204 kila mwezi alipokuwa ameajiriwa na mkewe na kuingiza jumla ya $554,465 mwaka jana kama meneja wake.
Blige alimpa Issacs $35,000 mwezi August na $50,000 September kama fedha za kujikimu (spousal support) pamoja na $25,000 kulipa wanasheria.
3978d11200000578-3845996-image-a-30_1476754603607
Kwenye nyaraka zake, Issacs anadai ameshazitumbua fedha hizo kwakuwa bado hajapata mahali pa kuishi na kwamba akaunti yake ya benki -$13,104.
Isaacs anataka pia apewe $5,000 ambazo huwalipa wazazi wake kila mwezi na $71,000 za kodi anazodaiwa!
“Issacs also pays nearly $5,000 a month in support for two children from a past relationship, $2,500 on auto expenses and transportation, $5,708 in maintenance and repair on his properties and another $5,732 on groceries.
He has also asked for help in paying the $21,677 he gives in charitable donations and the $10,000 he spends on entertainment, gifts and vacations,” wameandika Mail Online.

Download application yetu na upate habri punde zinapotufikia HAPA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni