.

Jumamosi, 16 Julai 2016

Islamic State wadai kushiriki shambulizi la Nice


Kundi la wapiganaji wa Islamic State limedai kuwa shambulio lililofanywa na mtu aliyewakanyaga watu na lori alikuwa mmoja wa wanachama wake.

Madai hayo yameonekana kwenye mtandao wa kundi hilo unaojulikana kama Amaq.

IS wamekuwa wakitumia mtandao huo kueneza propaganda zao.

Hata hivyo hakuna habari za kuthibitisha kuwa kundi hilo lilihusika moja kwa moja na shambulio hilo.

Tovuti hiyo ya Amaq imekuwa ikieneza taarifa ya IS inayohimiza waislamu kushambulia mtu au watu wanaotoka nchi za muungano wa mataifa yanayoshambulia kundi hilo.

Hata hivyo kuna wanaosema IS imetumia nafasi ya shambulio hilo kujikuza ingawa huenda kamwe hawakuhusika.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni