.

Jumanne, 24 Mei 2016

Nuh Mziwanda: Miaka Mitatu ya Kuwa na Shilole Imenipoteza Mambo Mengi


Nuh Mziwanda amedai katika miaka mitatu aliyokuwa na uhusiano na Shilole amepoteza mambo mengi.
Akiongea na Bongo5 Nuh amesema hakuna zaidi anachokumbuka kwenye uhusiano huo zaidi ya majuto.
“Kuna vitu muhimu sana ambavyo nimegundua ningeweza kuvifanya na ningekuwa nipo mbali sana,” amesema Nuh. Muimbaji huyo amesema uhusiano huo ulimfanya auchukulie poa muziki na hivyo kushindwa kutengeneza hit song.
Anasema Shilole alihakikisha katika muda wote waliokuwa nao Nuh asihit kwa uoga kuwa akiwa staa atamuacha.
“Yule [Shilole] alikuwa na trick nyingi za kunifanya mimi nijionee staa tayari, nijione mimi napendwa na watu au mimi muziki wangu unavuma kumbe bado halafu yeye huku muziki wake unaenda,” amesisitiza.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni